MKURUGENZI MKUU REA ASISITIZA UCHAPAKAZI KWA WATUMISHI
Na Veronica Simba - REA
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewataka wafanyakazi wote wa Taasisi hiyo kufanya kazi kwa weledi na kujituma ili kufikia malengo yake ya kuboresha maisha ya wananchi vijijini kwa kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na zenye gharama nafuu.
Aliyasema hayo mwishoni mwa juma, Julai 29, 2022 wakati wa kikao maalum baina yake na wafanyakazi wa REA kilicholenga kujadili utendaji kazi, kusikiliza changamoto za watumishi na kuzitolea majibu.
Mhandisi Saidy aliwataka wafanyakazi wote kushirikiana na kuweka nguvu ya pamoja katika utekelezaji wa vipaumbele vya Wakala kwa sasa, ambavyo alivibainisha kuwa ni pamoja na kupeleka umeme vitongojini, programu ya kusaidia upatikanaji wa petroli vijijini, mradi wa kuwezesha upatikanaji wa nishati bora ya kupikia vijijini pamoja na kupeleka umeme katika visiwa.
Kuhusu usambazaji umeme vitongojini, alieleza kuwa ni mradi unaolenga kuvipelekea umeme vitongoji vyote ambavyo havijafikiwa na nishati hiyo, baada ya kila kijiji sasa kufikiwa na mradi wa umeme.
Alifafanua kuwa gharama ya mradi inakadiriwa kuwa shilingi trilioni 6.5 na kwamba katika mwaka huu wa fedha, shilingi bilioni 140 zimetengwa kwa ajili ya utambuzi wa wigo wa mradi pamoja na kuanza kazi ya utekelezaji wa mradi awamu kwa awamu.
Vilevile, aliuelezea mradi wa kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kusambaza bidhaa za petroli vijijini, ambapo alibainisha kuwa Serikali imeubuni ikilenga kuwezesha na kuendeleza vituo hivyo kwa maeneo ya vijijini ambayo hayana vituo vya mafuta kwa njia ya mkopo nafuu.
Alisema kuwa mradi huo ni wa majaribio ambao ni sehemu ya jitihada za kutafuta mbinu bora zaidi za kusambaza nishati ya mafuta salama na kwa bei nafuu vijijini.
Pia, Mkurugenzi Mkuu alifafanua kuwa katika mwaka huu wa fedha, Serikali imetenga shilingi milioni 500 ili kufanya kampeni ya kuhamasisha matumizi ya nishati bora ya kupikia pamoja na kuwezesha kufanyika kwa tafiti za kubaini nishati, mfumo sahihi na vivutio vya kusambaza nishati hiyo kwa maeneo ya vijijini.
Aliongeza kuwa, katika mwaka wa fedha 2022/23, shilingi bilioni 10 zitatumika
MKURUGENZI MKUU REA ASISITIZA UCHAPAKAZI KWA WATUMISHI
Reviewed by Fahadi Msuya
on
July 31, 2022
Rating:
Reviewed by Fahadi Msuya
on
July 31, 2022
Rating:



Post a Comment