Tanzania kuendelea kuimarisha ushirikiano na Global Fund
Montreal , Canada, 30 Julai 2022.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi leo tarehe 30 Julai,2022 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Global Fund Bw. Peter Sand katika Mkutano wa Kimataifa wa UKIMWI unaofanyika Montreal nchini Canada.
Katika mazungumzo hayo Prof. Makubi amemuhakikishia Mkurugenzi huyo kuwa Wizara ya Afya itaendelea kudumisha mahusiano ya karibu na mfuko huo pamoja na kusimamia kwa makini miradi pamoja na kuboresha zaidi huduma za afya kwa wananchi.
Katika Mkutano huo Tanzania imewasilisha 360 video ya mafanikio ya mfuko wa Serikali na Global Fund katika kudhibiti magonjwa ikiwemo UKIMWI, Malaria, TB na kuimarisha mifumo ya Afya.
Mkurugenzi Mkuu wa Global Fund ameahidi kutembelea Tanzania mwanzoni mwa mwezi Septemba mwaka huu.
Tanzania kuendelea kuimarisha ushirikiano na Global Fund
Reviewed by Fahadi Msuya
on
July 30, 2022
Rating:
Reviewed by Fahadi Msuya
on
July 30, 2022
Rating:



Post a Comment