VITENDO VYA UKATILI VYATAJWA KUWA TISHIO LA MAGONJWA YA AFYA YA AKILI
Na Yusuph Digossi
Watanzania wametakiwa kuungana kwa pamoja kupinga vitendo vya ukatili kwa Wanawake na watoto ambao husabisha kuongezeka kwa magonjwa ya afya ya akili kwa wahanga wa vitendo hivyo
Wito huo umetolewa na Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi maalumu Dkt. Nandera Ernest Mhando wakati akifungua Kongamano la Tisa la Kisayansi kuhusu Magonjwa ya Afya ya Akili na Ukatili liloandaliwa na Chuo Cha Sayansi Shirikishi Muhimbili leo Jumatano Septemba 14 Jijini Dar es Salaam.
Dkt Nandera amesema kuwa Asilimia 70 ya Wanawake hufanyiwa vitendo vya ukatili hivyo Jamii inatakiwa kuunga Mkono juhudi za Serikali na wanaharakati kukemea vitendo hivyo.
"Kuzungumzia Changamoto za Ukatili na ugonjwa wa Afya ya akili ni wajibu wa tafiti na ujumuishi wa wadau mbali mbali”. amesema Dkt Nandera
Awali akimkaribisha DK. Nandera Mhando ili kufungua kongamano Hilo. Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha afya na sayansi shirikishi, Muhimbili Prof.Bruno Sunguya amesema lengo la kongamano hilo Ni kukutanisha wadau mbalimbali wa magonjwa ya akili na ukatili nchini ili kupokea matokeo mbalimbali ya Tafiti za Kisayansi na kuyafanyia uchambuzi wa kina.
VITENDO VYA UKATILI VYATAJWA KUWA TISHIO LA MAGONJWA YA AFYA YA AKILI
Reviewed by Fahadi Msuya
on
September 14, 2022
Rating:
Reviewed by Fahadi Msuya
on
September 14, 2022
Rating:





Post a Comment