Header AD

header ads

Waziri Mchengerwa aipongeza Yanga Kwa kuendeleza ubingwa ligi ya mabingwa wa Afrika



Na John Mapepele 

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameipongeza Timu ya Yanga  kwa kushinda kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga imeshinda  mabao 5-0 dhidi ya timu Zalan FC ya Sudani Kusini katika mchezo wa marudiani uliochezwa leo Septemba 17, 2022 kwenye uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.


Amesema watanzania na wanachama  wa Yanga wanafurahi kuona wanafanya vizuri  katika  mashindano haya ambapo amefafanua kuwa Mhe. Rais  pia anaipongeza  timu hiyo.

Amesema timu hiyo imeonyesha uzalendo ambao unapaswa kuendelezwa ili kuitangaza Tanzania Kimataifa.

Ameitaka timu hiyo kutoridhika na ushindi walioupata leo na badala yake iendelee kufanya mazoezi zaidi ili kujinoa hatimaye timu hiyo iingie fainali na kuweza kurejesha kombe nyumbani.


"Ninatoa wito kwa timu yetu kutobweteka na ushindi  tulioupata leo, watanzania wanakiu ya ubingwa wa kombe hili. Tunahitaji kujituma na kutanguliza uzalendo ili tuwape raha watanzania". Amesisitiza Mhe. Mchengerwa

Yanga  imerudiana  na Zalan FC leo Septemba 17, 2022 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kama wenyeji wakati Simba itarudiana kesho Septemba 18, 2922 katika Uwanja huu huu wa Mkapa jijini Dar es Salaam katika mashindano hayo hayo na  Nyasa Big bullet ya Malawi.

Kapteni   wa Timu hiyo Bakari Mwamnyeto amesema  huu ni mwanzo wa kutwaa ushindi ambapo amesema timu yake imejizatiti  kuchukua  kombe hilo


Waziri Mchengerwa aipongeza Yanga Kwa kuendeleza ubingwa ligi ya mabingwa wa Afrika Waziri Mchengerwa aipongeza Yanga Kwa kuendeleza  ubingwa ligi ya mabingwa wa Afrika Reviewed by Fahadi Msuya on September 17, 2022 Rating: 5