Header AD

header ads

Breaking news- Serengeti Girls yawaahidi watanzania ushindi




Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo. Mhe,  Mohamed Mchengerwa ameitakia kila la kheri timu ya Serengeti Girls katika mashindano ya Kombe la Dunia yanayoanza leo nchini India huku ikitarajia kutupa karata yake ya kwanza majira ya saa 11:30 jioni leo dhidi ya timu ya Japan, huku timu hiyo ikiwaahidi watanzania ushindi.

Akiongea leo muda mfupi kabla ya kuanza mechi hii,   Mhe. Mchengerwa amesema Mhe. Rais na watanzania wanafuatilia  kwa karibu na  wanamatumaini  makubwa na  timu hiyo na kuwataka kucheza kufa na kupona ili kurejesha kombe hilo nyumbani.

"Mimi kama Waziri sitarajii kusikia kuwa mmetolewa, ninachotaka  kusikia ni nyie kurudi na kombe nyumbani. Mhe Rais ana matarajio makubwa " amesisitiza, Mhe. Mchengerwa

Amefafanua kuwa Serikali inatumaini kuwa timu hiyo inakwenda kufanya vizuri zaidi kuliko timu ya Soka ya Taifa ya wenye ulemavu (Tembo Warriors) iliyofuzu kuingia robo fainali na kuiletea Tanzania heshima kubwa.

Aidha, amewataka wachezaji kuonesha viwango vya juu katika mashindano haya ili  waweze kununuliwa na vilabu vikubwa duniani.
 
Pia Mhe. Waziri amewataka viongozi  walioambatana  na timu hiyo kusimamia  kikamilifu jukumu walilopewa na taifa na kuhakikisha kuwa timu  inakuwa na hamasa kubwa na inashinda.

Amesema  dhamira Serikali kwa sasa ni kuibua vipaji vya vijana na kuwaomba watanzania kuiombea timu hii ili ushinde.

Nahodha wa timu hiyo Noela Luhala amemhakikishia Mhe. Waziri Mchengerwa  kuwa timu yake inakwenda kupambana kufa na kupona  kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mashindano ili kulinda heshima ya Rais na watanzania  hatimaye kurejesha kombe nchini.
Breaking news- Serengeti Girls yawaahidi watanzania ushindi Breaking news- Serengeti Girls yawaahidi watanzania  ushindi Reviewed by Fahadi Msuya on October 12, 2022 Rating: 5