Header AD

header ads

Waziri Mchengerwa awapongeza Serengeti Girls Kwa kuibamiza Ufaransa.





Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameipongeza timu ya Soka ya Wanawake Serengeti Girls Kwa kuibamiza  timu ya Ufaransa  mabao 2-1  katika mashindano ya Kombe la Dunia yanayoendelea nchini India.

Mhe. Mchengerwa amesema wachezaji wameonesha uzalendo mkubwa kwa nchi yao na amewataka kuendelea kucheza kufa na kupona  katika mechi zilizosalia ili  kurejesha kombe nyumbani.

Aidha, amesisitiza kuwa Serikali ipo pamoja na timu hiyo katika kila hatua  ili kuhakikisha inarudi na kombe nchini.

Amewaomba watanzania kwa umoja wao waiombee timu hiyo ili  hatimaye ishinde mechi zilizobaki. Na kutwaa  kombe.

Magoli ya  Tanzania yamefungwa na Diana Mnaly na Christer  Bahela.

Kwa matokeo hayo Tanzania inakamata namba 2 nyuma ya Japan na nafasi ya tatu Canada na nne ni  Ufaransa, huku ikiwa na mechi Moja mkononi dhidi ya Canada itakayochezwa Oktoba 18, 2022 jijini Mumbai, India.

Mhe. Mchengerwa ametoa wito kwa 
Uchungizi  umebaini  wananchi wengi nchini wamekuwa wakifuatilia mtanange  huo, huku wakiwaombea  waendelee kushinda.


Waziri Mchengerwa awapongeza Serengeti Girls Kwa kuibamiza Ufaransa. Waziri Mchengerwa awapongeza Serengeti Girls Kwa kuibamiza Ufaransa. Reviewed by Fahadi Msuya on October 15, 2022 Rating: 5