Header AD

header ads

NBAA YAKAGUA MAKAMPUNI 402 YA UKAGUZI, YAADHIMISHA MIAKA 50 TANGU KUANZISHWA KWAKE

Mwenyekiti kamati ya maandalizi ya sherehe za miaka 50 ya NBAA CPA Dr. Neema Kiure akielezea jambo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA CPA Pius A. Maneno katika ufunguzi wa maonesho ya huduma za kihasibu katika uwanja wa Mnazi Mmoja.


Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA CPA Pius A. Maneno akisaini kitabu cha mahudhurio baada ya kutembelea banda la NBAA katika ufunguzi wa maonesho ya huduma za kihasibu katika uwanja wa Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
Afisa masoko wa TBS Rhoda Mayugu  akimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA CPA Pius Maneno  mara baada ya kutembelea banda la TBS katika maonesho ya miaka 50 ya  NBAA yaliyofunguliwa rasmi leo Alhamisi Novemba 10 katika viwanja vya mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam 


Na Yusuph Digossi - Sauti za Mtaa Blog

Dar es salaam

Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (​NBAA) imesema kuwa itaendelea kushirikiana na serikali na wadau wa nje na ndani kuhakikisha Tanzania inakua na maendeleo katika fani ya uhasibu, fedha na huduma nyinginezo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA CPA Pius Maneno wakati akifungua maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya NBAA katika viwanja vya mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam .

CPA Maneno amesema NBAA imeweza kuishauri Serikali katika masuala ya kodi haswa kwenye maboresho na kuongeza wigo wa kodi na kupunguza ambazo zinaharibu jamii .

Ameeleza kuwa NBAA imeweza kukagua makampuni 402 ya ukaguzi na kampuni za simu 102 na kubainisha kuwa idadi ya Wanafunzi imeendelea kuongezeka ambapo kwa sasa kuna wanafunzi takribani 7000.

Amesema shughuli zote za NBAA zinafanyika kwa mfumo wa tehama isipokua shughuli moja ya usimamamizi wa mitihani kutokana na changamoto ya utamaduni wa Tanzania huku akibainisha kuwa changamoto hiyo inafanyiwa kazi.
NBAA YAKAGUA MAKAMPUNI 402 YA UKAGUZI, YAADHIMISHA MIAKA 50 TANGU KUANZISHWA KWAKE NBAA YAKAGUA MAKAMPUNI 402 YA UKAGUZI, YAADHIMISHA MIAKA 50 TANGU KUANZISHWA KWAKE Reviewed by Fahadi Msuya on November 11, 2022 Rating: 5