MILIONI 438,111,518.39 KUNUFAISHA VIKUNDI 24 MIKOPO ASILIMIA 10 MANISPAA YA KIGAMBONI
Hayo yamebainika leo 17/1/2023 wakati wa mahojiano na Mratibu Dawati la uwezeshaji wananchi kiuchumi anashughulikia masuala ya mikopo kwa vikundi vya wajasiliamali katika Idara ya Maendeleo ya jamii Manispaa ya Kigamboni ndg.Masesa Mgonela Luanda ambapo amesema tayari vikundi 24 vilivyokidhi vigezo vimeshapitishiwa mikopo yao na taratibu zote zimefuatwa hivyo watapokea fedha zao ili kutekeleza yale waliyoyapanga kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za ujasiriamali na kujiinua kiuchumi.
Akichanganua jinsi mgawanyo wa fedha hizo ulivyo kulingana na makundi ndg. Masesa amesema katika fedha hizo shilingi 211,265,411.34 zitaenda kwa vikundi 11 vya wanawake,shilingi milioni 131,265,411.34 zitaenda kwa vikundi 7 vya vijana na shilingi milioni 95,580,695.71 zitaenda kwa vikundi 6 vya watu wenye ulemavu.
Kuhusu urejeshaji wa mikopo hiyo ndugu Masesa anatoa wito kwa wanufaika wa mikopo hii kuwa fedha hizo sio zawadi inatakiwa kurejeshwa ili vikundi vingi zaidi viweze kunufaika kwani pesa zinavyorudi ndivyo zinavyosaidia kuwakopesha wengine na vikundi vingi vinapata kufaidika zaidi.
Mikopo hii ya asilimia kumi isiyo na riba hutolewa na kila halmashauri ambapo imewanufaisha na kuendelea kuwanufaisha makundi mbalimbali katika kujikwambua kiuchumi ikiwa ni dhamira thabiti ya serikali kuwakwamua wananchi kiuchumi na kuboresha maisha yao pamoja na kutekeleza Ilani ya CCM kivitendo.KAZI IENDELEE
Imetolewa na kitengo cha Mawasiliano Serikalini KGMC
MILIONI 438,111,518.39 KUNUFAISHA VIKUNDI 24 MIKOPO ASILIMIA 10 MANISPAA YA KIGAMBONI
Reviewed by Fahadi Msuya
on
January 17, 2023
Rating:
Reviewed by Fahadi Msuya
on
January 17, 2023
Rating:

Post a Comment