NMB Yawatambua wanafunzi Ubora na Kuimarisha Ushirikiano na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Benki ya NMB kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitivo cha Biashara, imewatambua wanafunzi kumi bora katika kozi kumi waliomaliza masomo mwaka huu kwa hafla maalum ya utoaji wa zawadi mbalimbali, ikiwatambua kwa mafanikio yao ya kitaaluma na juhudi kubwa iliyowaletea ufaulu.
Hafla iliyofanyika siku moja kabla ya kuanza kwa mahafali za chuo hicho, zawadi za pesa taslimu, vyeti na fursa za mafunzo kazini kwa washindi hao zilitolewa na Benki ya NMB huku wawakilishi wa Benki hiyo wakipongeza juhudi kubwa za wahitimu na chuo kwa ujumla katika dhamira yao ya kukuza vipaji na maendeleo ya kitaalamu.
Kwa niaba ya Benki ya NMB, Mgeni Rasmi wa shuguli hiyo, Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu, Kituo cha Utaalamu wa Benki ya NMB, Joanitha Mrengo, alielezea fahari ya Benki katika kuunga mkono juhudi mbalimbali za vijana na hususani za kitaaluma ambazo zitazaa watalaamu bora kwa maslahi ya taifa kwa ujumla.
“Kwetu sisi ni fahari kubwa kushiriki katika kutambua bidii na juhudi za vijana hawa wadogo, alisema joanitha.
“Leo hii tunashuhudia nidhamu, uvumilivu na ubora wao wa kitaaluma ukileta majibu stahiki. Benki ya NMB itatengeneza fursa kuanzia za ajira na hata za mafunzo kazini ambazo tunaamini zitawawezesha wataalamu hawa kustawi katika soko la ajira.”
Mrengo aliongeza kuwa Benki ya NMB inaendelea kujivunia ushirikiano wa dhati uliopo baina ya taasisi hiyo ya fedha na chuo kikuu cha dar es salaam kwani wameshafanya mengi ikiwemo kutoa fursa za kuwapa wanafunzi nafasi za kujifunza wakiwa masomoni katika benki hiyo na hivyo kuchangia katika kuzalisha wataalamu zaidi katika sekta ya kifedha.
“Mbali na mafunzo wakiwa kazini watakayopata washindi wetu wa leo, tumekuwa na ushirikiano na Chuo kikuu cha Dar es Salaam katika kuendelea kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa chuo hiki. Lakini pia tunayo makubaliano makubwa ya kuendelea kushirikiana katika masuala ya kitehama,” Alisema Mrengo.
Naye Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Utafiti, Profesa Nelson Boniface, pia alisisitiza umuhimu wa ushirikiano huo akisema, “Ushirikiano wetu na Benki ya NMB.
Post a Comment