MAKAMU WA RAIS WA UGANDA MHE JESSICA ALUPO ATEMBELEA MAKUMBUSHO YA TAIFA
Makamu wa Rais wa Uganda Mhe Jessica Alupo ametembelea Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujionea na Urithi adhimu na adimu wa Historia ya Tanzania uliohifadhiwa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni.
Mhe Alupo alipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa Dkt Noel Lwoga, na kupatiwa maelezo ya Uhifadhi wa Uridhi wa Utamaduni na Historia kutoka kwa Wataalam wa Makumbusho hiyo.
Alikuja nchini kwa kuudhuria Mkutano wa Wanawake na Vijana katika biashara chini ya Mkataba wa Eneo huru la biashara Afrika uliofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, Jijini Dar es Salaam.
MAKAMU WA RAIS WA UGANDA MHE JESSICA ALUPO ATEMBELEA MAKUMBUSHO YA TAIFA
Reviewed by Fahadi Msuya
on
September 13, 2022
Rating:
Reviewed by Fahadi Msuya
on
September 13, 2022
Rating:




Post a Comment