Header AD

header ads

RASIMU YA MTAALA YAWASILISHWA KWA WADAU




Kamati ya Kitaifa ya Uboreshaji Mitaala leo tarehe 27/09/2022 imewasilisha rasimu pendekezwa ya mitaala ya Elimu ya Awali, ElimuMsingi, Sekondari na Elimu ya Ualimu kwa wadau mbalimbali wa Elimu.

Kikao hicho  kimefanyika Jijini Dodoma katika ukumbi wa Tume ya Uchaguzi na kuhudhuriwa na Wabunge, Timu ya Zanzibar inayoshughulikia  Sera na Mitaala, Vyuo Vikuu, Taasisi za Dini, BAKITA, Wadau wa Maendeleo na Wathibiti ubora wa shule.

Mapendekezo ya Rasimu yamewasilishwa na Mwenyekiti wa Kamati Prof. Makenya Maboko na Kamati imepokea maoni mbalimbali kutoka wa wadau na kuahidi kuyafanyia kazi katika maboresho ya Mitaala yanayoendelea.



RASIMU YA MTAALA YAWASILISHWA KWA WADAU RASIMU YA MTAALA YAWASILISHWA KWA WADAU Reviewed by Fahadi Msuya on September 27, 2022 Rating: 5