Header AD

header ads

WAZIRI MCHENGERWA- SERIKALI KUMWAGA VIWANJA VYA KIMATAIFA KILA KONA.




Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Serikali kupitia Wizara anayoiongoza inakwenda kukarabati viwanja vyake katika kiwango cha kimataifa ili viweze kutumika kwenye mashindano  ya kimataifa.


Mhe.  Mchengerwa ametoa kauli hiyo leo Bungeni wakati akitoa majibu ya nyongeza kwenye swali aliloliuliza na Mhe. Festo Sanga, Mbunge wa Makete aliyetaka kujua fedha iliyopitishwa na Serikali kwa ajili ya kuweka nyasi bandia kwenye   viwanja vya michezo.


Amesema dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuhakikisha kuwa miundombinu ya michezo inaboreshwa na inakuwa ya kisasa zaidi. 


Viwanja ambavyo  vilipangiwa  kukarabatiwa ni pamoja na  viwanja vya Benjamini Mkapa, na uhuru vya Jijini Dar es Salaam, Arusha, Tanga, Mwanza, Mbeya  na Dodoma.


 Mbali na kufanya ukarabati wa viwanja hivyo pia serikali inakwenda kutengeneza miundombinu ya michezo kwenye shule mbili katika kila mkoa ili kuibua vipaji vya michezo.


Aidha, tayari Mhe. Waziri kwenye mikutano kadhaa na wadau wa michezo ikiwa ni pamoja na Kikao cha wadau wa Baraza la Michezo na kikao cha viongozi wa vilabu vya michezo amehimiza kila timu kuwa na   kiwanja  cha  michezo kulingana na matakwa ya sera ya michezo ambapo vilabu  vyote  vilikubali kuwasilisha  mpango wa ujenzi WA viwanja hivyo katika kipindi cha miezi sita kuanzia mwezi Agosti mwaka huu.


WAZIRI MCHENGERWA- SERIKALI KUMWAGA VIWANJA VYA KIMATAIFA KILA KONA. WAZIRI MCHENGERWA- SERIKALI  KUMWAGA VIWANJA VYA KIMATAIFA KILA KONA. Reviewed by Fahadi Msuya on September 13, 2022 Rating: 5