Header AD

header ads

MKENDA ARIDHISHWA NA KIWANDA DARASA DIT




Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza vipuri vya vyombo vya moto unaofanywa na Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT).

Waziri ametembelea kiwanda hicho cha kujifunzia leo kuona hatua iliyofikiwa. Kiwanda hicho  kinatarajiwa kufunguliwa rasmi kitakapo kamilika.


Prof. Mkenda  ameridhishwa na uwekezaji na maboresho yaliyofanyika ambapo amesema kuna mabadiliko mengi mazuri yamefanyika tofauti na alipotembelea  mwezi julai. 

"Nimeridhishwa  na uboreshaji ulifanyika mpaka sasa, kutoka kwenye utengenezaji wa Vipuri vya bajaji pekee mpaka vipuri vya magari hongereni sana hii ni hatua nzuri," amesema.


Prof. Mkenda amesisitiza kuwa  DIT kupitia kampuni Tanzu ya taasisi hiyo (DIT Company Ltd) ifuate taratibu zote ili kuhakikisha hatimiliki inapatikana kwa ajili ya kazi ya uzalishaji inayofanywa kupuka bunifu hizo kuibiwa.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi,  Mhandisi Dkt. Richard Masika amesema pamoja na kutengeneza vipuri, DIT inatarajia kutengeneza na kuuza mashine za kutengenezea vipuri ili kuweza kukidhi mahitaji ya soko.


MKENDA ARIDHISHWA NA KIWANDA DARASA DIT MKENDA ARIDHISHWA NA KIWANDA DARASA DIT Reviewed by Fahadi Msuya on December 02, 2022 Rating: 5