Header AD

header ads

Mhe. Mchengerwa ampongeza Simbu kutwa medali ya fedha , Jumuiya ya Madola



Na John Mapepele, Uingereza.


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amempongeza mwanariadha Alphonse Felix Simbu  kwa kushika nafasi ya  pili na Hamis Mesai kushika nafasi ya nane kwenye mashindano ya mbio za Marathoni ya Jumuiya ya Madola yanayoendelea nchini Uingereza.

Mhe. Mchengerwa amesema kazi ushindi  Simbu ni wa watanzania  wote ambapo amewataka wanamichezo wote wanaoshiriki mashindano hayo kutanguliza uzalendo ili kuipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa.


Kufuatia ushindi huo Simbu anajinyakulia zawadi ya dola za kimarekani 7500 kutoka Serikalini ikiwa ni ahadi aliyoitoa waziri Mchengerwa wakati akiiaga timu ya Tanzania.

Mara baada ya kushinda Simbu amesema anawashukuru watanzania kwa maombi yao ambayo yamemfanya ashinde katika mashindano hayo.

Amesema siri ya ushindi ni mazoezi ambapo amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mchengerwa  kwa kutoa msukumo wa pekee kwenye michezo.


Mhe. Mchengerwa ampongeza Simbu kutwa medali ya fedha , Jumuiya ya Madola Mhe. Mchengerwa ampongeza Simbu kutwa medali ya fedha , Jumuiya ya Madola Reviewed by Fahadi Msuya on July 30, 2022 Rating: 5