Mhe. Mchengerwa ampongeza Simbu kutwa medali ya fedha , Jumuiya ya Madola
Na John Mapepele, Uingereza.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amempongeza mwanariadha Alphonse Felix Simbu kwa kushika nafasi ya pili na Hamis Mesai kushika nafasi ya nane kwenye mashindano ya mbio za Marathoni ya Jumuiya ya Madola yanayoendelea nchini Uingereza.
Mhe. Mchengerwa amesema kazi ushindi Simbu ni wa watanzania wote ambapo amewataka wanamichezo wote wanaoshiriki mashindano hayo kutanguliza uzalendo ili kuipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa.
Kufuatia ushindi huo Simbu anajinyakulia zawadi ya dola za kimarekani 7500 kutoka Serikalini ikiwa ni ahadi aliyoitoa waziri Mchengerwa wakati akiiaga timu ya Tanzania.
Mara baada ya kushinda Simbu amesema anawashukuru watanzania kwa maombi yao ambayo yamemfanya ashinde katika mashindano hayo.
Amesema siri ya ushindi ni mazoezi ambapo amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mchengerwa kwa kutoa msukumo wa pekee kwenye michezo.
Mhe. Mchengerwa ampongeza Simbu kutwa medali ya fedha , Jumuiya ya Madola
Reviewed by Fahadi Msuya
on
July 30, 2022
Rating:
Reviewed by Fahadi Msuya
on
July 30, 2022
Rating:



Post a Comment