Header AD

header ads

HANDENI , KILINDI ZATAJWA KUONGOZA UTENGENEZAJI SILAHA ZA MOTO



Na Hadija Bagasha Tanga, 


Wilaya ya Handeni na Kilindi zimetajwa kama wilaya zinazoongoza kwenye utengenezaji wa silaha za moto jambo ambalo limekuwa likihatarisha usalama wa watu sambamba na wanyama kwenye hifadhi za Taifa zinazopakana na maeneo hayo ikiwemo tembo. 

Kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga Safia Jongo ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kusalimisha silaha haramu kwa hiari iliyofanyika Mkoani Tanga na kushirikisha wadau mbalimbali wa usalama. 


"Handeni Kilindi wazigua wenzangu wana tabia ya kumiliki gobole kama mlinzi wanazitengeneza wenyewe hilo gobole umelitengeneza lakini unalimiki kinyume na visivyo halali wakati muafaka umefika isalimishe silaha yako kwa Mwenyekiti wa serikali za mtaa mwambie mimi nilichonga gobole kama mila lakini kwa sasa ninajua sio halali naiwasilisha silaha hii, "alisema Kamanda Jongo. 

Kamanda Jongo amesema urejeshaji wa silaha hizo utamsaidia mmiliki mwenyewe pamoja na jamii kwasababu kumiliki silaha isivyo halali kunaweza kuchangia kufanyika kwa matendo ya uhalifu wa watu kwa kutumia silaha panoja na wanyama. 


Kamanda Jongo alibainisha kuwa  kumekuwa na matukio mbalimbali yanayohusishwa na matumizi ya silaha kinyume cha sheria  ikiwemo mauaji ya wanyama na mengine ya kiuhalifu ambapo katika jitihada walizoendelea kuzichukuwa  walifanikiwa kukamata silaha 62  na watuhumiwa 63 wakikamatwa kwa kipindi cha kuanzia January  Hadi june 2022.

Jongo alisema kufwatilia uzagaaji wa silaha Tanga ni miongoni mwa mikoa mabayo unaweza kuathirika  moja kwa moja katika mauaji na uwindaji haramu wa wanyama mbalimbali .


"Tanga itakuwa ni moja wapo ya mikoa ambayo itaathirika  endapo  kutakuwa na uzagaaji wa silaha kwani kutakuwa na vitendo vya uhalifu  Kama mauaji na uwindaji haramu, mapori yetu mengi Yana wanyama silaha hizo zimekuwa zikitengenezwa kienyeji ,  kwahiyo urasimishaji wa silaha utatusaidia  na utajisaidia mwenyewe na kjisaidia jamii kwa sababu kumiliki silaha visivyo halali utafanya matendo ambayo yatatuletea  shida Kama uhalifu wa wanyama na matukio mengi ambayo yanatumia silaha" alisema Jongo.

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha usimamizi na udhibiti wa silaha na leseni makao makuu ya jeshi la polisi Renada Milanzi amesema silaha zinazosalimishwa ni pamoja na zilizoingizwa nchini kinyume na sheria.



Milanzi amesema kuwa katika kuendelea kuimarisha ulinzi na usalama hapa nchini hatua za maksudi zimechukuliwa kwa kushirikiana  makundi mbalimbali  katika kutekeleza kampeni hiyo baada ya serikali kutoa tangqzo la msamaha  kwa yeyote atakayesalimisha silaha kwa hairi hatoshitakiwa.

"Jukumu la usalama ni la kila mwananchi hivyo Basi Polisi kwa kushirikiana na wadua wa ndani na nje kimeona umuhimu wa kuwashirikisha makundi mbalimbali katika jamii ili kutekeleza kampeni ya mwezi wa msamaha wa kurasimisha silaha kwa hairi ili kuimarisha usalama wa Taifa letu  kampeni hii inaendelea nchi nzima na atakayesalimisha hatoshitakiwa


Awali akizindua kampeni hiyo kwa niaba ya Mkuu wa MKoa Tanga Omari Mgumba, Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Kanal Maulid Sulumbu amesema zoezi hilo linalenga kuimarisha hali ya usalama nchini. 

Kanal Sulumbu amesema silaha haramu ndio chanzo kikubwa cha kuvunja amani na kurudisha maendeleo nyuma hivyo jamii inapaswa kushirikiana na jeshi la polisi kuzifichua silaha hizo. 


Jeshi la polisi Nchini limetoa msamaha kwa wamikili wa silaha haramu Nchini Tanzania na kuwataka wale wote wanaomiliki silaha kinyume na sheria kuzisalimisha kwa hiari yao kabla sheria haijachukua mkondo wake. 

Mkoa wa Tanga ni moja kati ya mikoa mitatu iliyochaguliwa kama Mkoa darasa kwenye kampeni za Mwaka 2022 huku Mikoa mingine ikiwa ni Morogoro na Tabora. 

Zoezi hilo ambalo ni kwa mara ya pili kufanyika hapa nchini kuanzia mwaka huu lilizinduliwa na Naibu waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Jumaanne  Abdallah  jijini Dodoma September 1 ambapo litendelea hadi October 31 , 2022. 



HANDENI , KILINDI ZATAJWA KUONGOZA UTENGENEZAJI SILAHA ZA MOTO HANDENI , KILINDI ZATAJWA KUONGOZA UTENGENEZAJI SILAHA ZA MOTO Reviewed by Fahadi Msuya on September 12, 2022 Rating: 5