Header AD

header ads

Waziri Mchengerwa Atembelea Eneo la Filamu za Ertugrul na Kurulus Osman





Waziri wa Utamaduno, Sanaa na Michezo, Mhe Mohamed Mchengerwa leo Oktoba 4, 2022, ametembelea eneo mashuhuri la uigizaji wa filamu nchini Uturuki chini ya mwongozaji mahiri wa filamu Mehmet Bosdaq, Bosdaq Film.

Mehmet na kampuni hiyo ndio wazalishaji wa filamu mashuhuri zinazorushwa nchini za Dirilis Ertugrul na Kurulus Osman (the Ottoman).

Katika ziara hiyo ambayo wamekubaliana kushirikiana kusaidia kuinua sekta ya filamu nchini Tanzania, Mhe Waziri ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Balozi Lt. Generali Yacoub Mohammed na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi.



Waziri Mchengerwa Atembelea Eneo la Filamu za Ertugrul na Kurulus Osman Waziri Mchengerwa Atembelea Eneo la Filamu za  Ertugrul na Kurulus Osman Reviewed by Fahadi Msuya on October 04, 2022 Rating: 5